Bi Joyce
Kasambala (70) mkaziwaMpwapwamkoani Dodoma akisoma machapisho mbalimbali yanayotolewa naTume ya Mabadiliko ya Katiba
wakati wa sherehe za Siku ya Wakulima Nanenane zilizofanyika hivi
karibuni katika viwanja vya Nzunguni mjini Dodoma.
Watoto
hawa Saada Yusuph (7) kushoto na mwenzake Joseph Makwate (8) wa kata ya
Nzunguni Manispaa ya Dodoma mjini wakisoma nakala za Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania wakati walipotembelea banda la Tume ya
Mabadiliko ya Katiba katika sherehe ya siku ya Wakulima Nanenane
zilizofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Nzunguni mjini Dodoma.
Wakazi
wa Manispaa ya mji wa Dodoma wakiwa katika foleni kusubiri kuingia
katika Banda la Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati wa kilele cha siku
ya Wakulima Nanenane zilizofanyika hivi karibuni katika viwanja vya
Nzunguni mjini humo.
KatibuwaJukwaa
la Wahariri(TEF) Neville Meenaakichangia hoja wakati wa mkutano wa
kubadilisha na mawazo baina ya Uongozi wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
na Baraza la Habari Tanzania (MCT) pamoja na Jukwaa la Wahariri
uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Waziri Mkuu mstaafu Jaji
Joseph Warioba, Katibu waTume Assaa Rashid na Naibu Katibu Casmir Kyuki.Picha Zote na Tume ya Mabadiliko ya Katiba