Friday, August 17, 2012

MIILI YOTE YA ASKARI SABA WA UGANDA WALIOKUFA KATIKA AJALI ZA HELKOPTA NCHINI KENYA YAPATIKANA.


Timu za waokoaji katika Mlima Kenya wamefanikiwa kupata miili minne ya mwisho ya askari wa Jeshi la Ulinzi la Uganda waliopata ajali na kuungulia ndani ya helkopta.
Jeshi la Ulinzi la Kenya limesema miili hiyo imesafirishwa kuelekea Nairobi kutoka eneo la tukio, na kukamilisha zoezi lililodumu kwa siku tatu la kutafuta na kuoko.
Idadi hiyi inafanya waliokufa katika ajali ya helkopta za Uganda zilizoanguka katika maeneo ya Mlima Kenya nchini Kenya kuwa saba (7).