Wednesday, March 30, 2016

WAZIRI NAPE ATEUA WAJUMBE WA KAMATI YA MAUDHUI



WAZIRI NAPE ATEUA WAJUMBE WA KAMATI YA MAUDHUI
Na Chalila Kibuda, Globu  ya Jamii.
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amewateua wajumbe wanne wa kamati ya maudhui watakaotumikia kipindi cha miaka mitatu.

Taarifa iliyotolewa  leo kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari Maelezo ilieleza kuwa uteuzi huo hufanyika kila baada ya miaka mitatu.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni  Joseph Mapunda ambaye ni  mhariri Mtendaji Mstaafu wa Magazeti ya Serikali(TSN) na  Mkurugenzi Mstaafu wa Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) Abdul Ngalawa.

Wengine ni  Mwandishi wa habari ,Mhadhiri Derek Murusuri  pamoja na Mwandishi wa habari ,Mwanasheria , Zainabu Mwatawala.