Kiongozi wa kampeni ya Okoa Tembo wa Tanzania,Shubert Mwarabu akizungumza na Waandishi wa habari ndani ya ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO,kuhusiana na Barua yao ya Wazi kwa Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli juu ya mauaji ya Tembo ambayo yamekuwa yakifanyika hapa nchini kwa kiwango kikubwa.Katika barua hiyo ya wazi,uongozi wa kampeni hiyo umetoa wito kwa Serikali kutekeleza ama kufanya yafuatayo1.kuwakamata na kuwashitaki wafanyabishara wakubwa wa meno ya Tembo nchini,bila kujali Utaifa,Hadhi au Mamlaka.2.Kutumia urafiki wa kihistoria kati ya Tanzania na China kufunga masoko ya meno ya Tembo huko china.3.Kuteketeza hadharani ghala ya meno ya Tembo Tanzania-inayosadikika kuwa kubwa kuliko yote Ulimwenguni.
Bwa.Shubert ameeleza kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika uhifadhi wa Tembo hapo kapla,anasema Mwaka 1989,Tanzania iliongoza jitihada za kupiga marufuku biashara ya mene ya Tembo Ulimwengu, "tulipochukua hatua kukomesha mauaji ya Tembo,Dunia nzima ilituunga mkono,hivyo ni lazima turejeshe upya dhamira yetu kwa ahadi tuliyojiwekea kwa hatua ya Kimataifa zaid ya miaka ishirini iliyopita,na kuleta ukomo wa biashara yote ya meno ya tembo hapa nchini'',alieleza Bwa.Shubert.

Pichani kati ni mmoja wa Wajumbe wa kampeni ya OKOA TEMBO WA TANZANIA,Bwa.Lameck Mkubulo akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari,kwenye mkutano uliofanyika mapema leo subuhi Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar,kuhusiana na Barua yao ya Wazi waliomuandikia Rais ya kumtaka achukue hatua juu ya suala la kupungua kwa kasi idadi ya Tembo nchini,kutokana na ujangili kwa ajili ya biashara haramu ya meno ya Tembo