Usiku wa kuamkia Jumatatu ya tarehe Aprili 20 mwaka huu, vijana kutoka Chuo cha Pasiansi kilichopo Serengeti kwa kushirikiana Kampuni ya Grumeti, walifanikiwa kukamata majangili watatu wakiwa na nyama ya swala aliyenaswa kwenye hifadhi ya Serengeti.
Baada ya kukamatwa, majangili hao walipandishwa kwenye gari la polisi na kupelekwa kituo cha Polisi cha Bunda.
Hii ni oparesheni endelevu katika Hifadhi ya Seregenti ambapo kila wiki majangili kadhaa wanakamatwa na kufikishwa mahakama maalum ya majangili kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka na kuchukuliwa hatua za kisheria.