Mara baada ya mahakama kutoa uamuzi wake haraka , mwanasheria mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema, Mh Tundu Lisu alizungumza na vyombo vya habari kuhusu Chadema kutomtambua Mh Zitto kama mwanachama wa chama hicho.
Ili kusikia kauli ya Mh Zitto kuhusu suala hilo Mpekuzi ilifika katika ofisi ndogo za bunge zilizoko jijini Dar es Salaam na kumshuhudia Mh Zitto akiongoza vikao vya kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu ya mashirika ya uma PAC ambapo baada ya kumalizika kwa kikao hicho,Zitto alizungumzia maamuzi hayo ya mahakama na Chadema baada ya kuhojiwa na waandishi wa habari.
"Taarifa hizo hata mimi nimezisikia mitandaoni na katika vyombo vya habari.Sina taarifa rasmi ya kuvuliwa uanachama na nipo kazini kama mnavyoniona.....
"Hata kama chama kingekuwa kimeamua hivyo, bado kuna taratibu za kufuata. Wanatakiwa kumwandikia barua spika wa Bunge ili ajiridhishe juu ya maamuzi hayo na kisha awajibu.
"Pia, maamuzi ya kumvua ubunge au uanachama mtu flani hayafanywi na mtu mmoja, ni lazima kikao halali cha chama kikae na kuamua hivyo." Alisema Zitto Kabwe
Ili kusikia kauli ya Mh Zitto kuhusu suala hilo Mpekuzi ilifika katika ofisi ndogo za bunge zilizoko jijini Dar es Salaam na kumshuhudia Mh Zitto akiongoza vikao vya kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu ya mashirika ya uma PAC ambapo baada ya kumalizika kwa kikao hicho,Zitto alizungumzia maamuzi hayo ya mahakama na Chadema baada ya kuhojiwa na waandishi wa habari.
"Taarifa hizo hata mimi nimezisikia mitandaoni na katika vyombo vya habari.Sina taarifa rasmi ya kuvuliwa uanachama na nipo kazini kama mnavyoniona.....
"Hata kama chama kingekuwa kimeamua hivyo, bado kuna taratibu za kufuata. Wanatakiwa kumwandikia barua spika wa Bunge ili ajiridhishe juu ya maamuzi hayo na kisha awajibu.
"Pia, maamuzi ya kumvua ubunge au uanachama mtu flani hayafanywi na mtu mmoja, ni lazima kikao halali cha chama kikae na kuamua hivyo." Alisema Zitto Kabwe