Friday, January 23, 2015

Mwenyekiti anusurika kupigwa,asindikizwa na polisi



Mwenyekiti anususrika kupigwa,asindikizwa na polisi


 Wananchi wa kijiji cha Puma katika wilaya ya ikungi mkoani Singida wame mkataa mwenyekiti  wa kijiji hicho katika mkutano wake wa kwanza na kusababisha diwani wa kata hiyo  kwa kushirikiana na jeshi la polisi kuingilia kati na kufunga mkutano kabla ya wakati ili kumnusuru asipigwe na wananchi.
Wananchi hao waliokuwa na hasira wamesema hakuna sababu ya kuwa na mwenyekiti ambaye wananchi hawamkubali kwa sababu katika uchaguzi uliopita kulikuwa na udanganyifu katika upigaji kura,kutokana na hali hiyo wamesema ni bora kuachana na vyama vya siasa wachague mwenye kiti wa kimila ili kukisaidia kijiji cha puma kupata maendeleo.
 
Baada ya vurugu  kuongezeka diwani wa kata hiyo kwa tiketi ya CCM,Bwana ramadhani kulungu ilibidi kufunga kikao hicho ili kuweza kumnusuru mwenyekiti wa kijiji cha puma na kuwatuliza wananchi ilikusitokee uvunjifu wa amani.
 
Mwenyekiti wa kijiji cha puma  kwa tiketi ya CCM ,Bwana Sifa Joramu awali ambaye alishindwa kabisa kuendesha kikao chake ,baada ya jeshi la polisi kuingilia kati na kuamua kumsindikiza kwa ulinzi mkali huku wananchi waki mzomea na kusema hawamtaki,amesema hizo ni fujo za vyama vya upinzani lakini yeye  atahakikisha kazi anafanya kwa sababu yeye ndiye aliyeshinda na kuapishwa kwa kazi ya uwenyekiti wa kijiji cha puma. 
 
Kundi la watu waliamua kumfuata na kumbeba  juu kisha kumzungusha mitaani Bwana Hassan Chaimbo aliye gombea kwa tiketi ya CHADEMA na kushindwa kwa kupata kura mianne arobaini na nne dhidi ya  Bwana Sifa  Joramu alishinda uwenyekiti wa kijiji cha puma kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi uliofanyika mwishoni  mwaka jana na kupata kura mianne hamsini na saba.