Tuesday, October 21, 2014

WATANO WANUSURIKA KUFA KWA AJALI KIMARA, DAR


WATANO WANUSURIKA KUFA KWA AJALI KIMARA, DAR

Gari aina ya Mitsubishi Canter likiwa pembezoni mwa barabara baada ya ajali hiyo.

Muonekana wa gari hilo baada ya ajali.


Baadhi ya raia waliokuwa kwenye eneo la tukio


Polisi wakiwa eneo la tukio.
Watu watano wamenusurika kufa kwa ajali Kimara Dar es Salaam baada ya gari dogo aina ya Toyota Rav 4 iliyokuwa ikitokea Kimara kuelekea Ubungo kuhama upande wa pili wa barabara na kugongana uso kwa uso na gari aina ya Mitsubishi Canter na kusababisha dereva wa Canter kuumia vibaya na kukimbizwa hospitali.
Waliokuwa ndani ya Rav 4 walipata majeraha madogo. Ajali hiyo imetokana na kutereza kwa barabara baada ya mvua kunyesha.

(Habari/Picha na :Global Whatsapp