Saturday, October 11, 2014

RAIS SHEIN ATEUA MAKADHI WAPYA WA WILAYA


RAIS SHEIN ATEUA MAKADHI WAPYA WA WILAYA
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya Uteuzi wa Makadhi wa Wilaya za Unguja na Pemba.Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee Makadhi hao ni Sheikh Ali Haruna Ramadhan-Unguja na Sheikh Abubakar Ali Mohamed-Unguja.Wengine ni Mohamed Ramadhan Khamis-Unguja na Sheikh Omar Juma Othman-Pemba.Rais Shein amefanya Uteuzi huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu namba 5 cha Sheria ya Mhakama ya Kadhi Namba 3 ya mwaka 1985 kama ilivyorekebishwa na Sheria namba 4 ya mwaka 2003.
Uteuzi huo umeanza Septemba 12,2014
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR