Saturday, September 13, 2014

TPDC, KAMPUNI ZA WENTWORTH, MAUREL & PROM WASAINI MKATABA WA KUUZIANA GESI


TPDC, KAMPUNI ZA WENTWORTH, MAUREL & PROM WASAINI MKATABA WA KUUZIANA GESI
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (wa nne kushoto) akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya WENTWORTH inayochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara , Robert MacBean (wa tatu kushoto) mara baada ya kusaini Makubaliano ya Mkataba wa Kuuziana Gesi kati yake na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Wengine katika picha ni baadhi wa Watendaji Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC na wawakilishi wa kampuni za WENTWORTH na MAUREL & PROM.
Wajumbe waliohudhuria kikao cha Kusaini Mkataba wa Kuuziana Gesi kati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na Kampuni zinazochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara za WENTWORTH Resources Limited na MAUREL & PROM wakisaini MKataba huo. Anayeshuhudia mbele ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo pamoja na wawakilishi wengine kutoka kampuni hizo, TPDC, Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) James Andilile (wa kwanza kulia) wakipitia Mkataba kwa pamoja na mmoja wa wawakilishi wa Kampuni hizo wakati wa kusaini Mkataba huo. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya MAUREL & PROM, Michael Hochard na wa kwanza ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya WENTWORTH Robert MacBean.