Mhe. Waziri Fatma Fereji                kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Serikali ya                Mapinduzi Zanzibar akizungumza kwa niaba ya Jamhuri ya                Muungano wa Tanzania wakati wa Kikao Maalum cha Baraza kuu                la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Jumatatu ambapo wakuu                wa nchi na wawakilishi wa serikali kutoka nchi 193                walikutana kutathimini Mpango wa Utekelezaji walioupitisha                miaka 20 iliyopita huko Cairo, Misri kuhusu uboreshaji wa                maisha ya watu na masuala yahusuyo Idadi ya Watu. Mhe.                Fereji ni sehemu ya Ujumbe wa Mhe. Rais Jakaya Mrisho                Kikwete katika Mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la Umoja wa                Mataifa. 
                Mhe. Waziri Fatma Fereji                akiwa na Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa                Mataifa, Balozi Tuvako Manongi na Naibu wake, Balozi                Ramadhan Mwinyi wakati wa ufunguzi wa Kikao Maalum wa ICPD                ambapo Waziri Fereji aliongoza ujumbe wa Tanzania katika                Mkutano huo. 
                Kutoka kushoto ni Balozi                Ramadhan Mwinyi, Waziri Fatma Fereji wakiwa na Mwakilishi                kutoka Ofisi za UNFPA ambaye aliwahi pia kufanya kazi                nchini Tanzania akimpongeza Waziri baada ya kutoa mchango                wa Tanzania na kulia kabisa ni Dkt. Joyceline Kaganda.