Wednesday, September 17, 2014

Mahakama ya Umoja wa Mataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (UN-ICTR) Yatoa Msaada wa Kompyuta Arusha



Mahakama ya Umoja wa Mataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (UN-ICTR) Yatoa Msaada wa Kompyuta Arusha
Mahakama ya Umoja wa Mataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (UN-ICTR) leo imetoa msaada wa Kompyuta 22, Monitor 154 na Printers 66 kwa mashule, vyuo, vituo vya afya, mashirika yasiyo ya serikali na taasisi zakidini na kijamii pamoja na idara za serikali katika jitihada zake za kusaidia jumuiya ya Kitanzania ambayo imeweza kuilea mahakama hiyo nchini kwa miaka karibu 20 sasa. 

Ofisi ya ya Mkuu wa Mkoa yenyewe iliongezewa gari moja la deraya na ulinzi. Makabidhiano hayo yalifanya mjini Arusha na viongozi wa UN-ICTR kwa wawakilishi wa wafadhiliwa hao katika sherehe fupi zilizofanyika kwenye uwanja wa rumande ya mahakama hiyo Kisongo.

Huu ni mwendelezo wa mahakama hiyo kuisaidia jamii hasa ya Arusha katika kipindi hiki ambapo imo mbioni kumaliza shunguli zake za kuwahukumu wale wote walioongoza mauaji hayo nchini Rwanda mwaka 1994. Taasisi na mashirika hayo yalikabidhiwa kila moja Computer moja, printer saba na monitor tatu. 
 Waliokabidhiwa ni; ABC Vocational Training Centre; Ambassador of Hope Netowrk of People with HIV/AIDS; Arusha Charity Pre and Primary School; Caucus of Children's Rights; Costigan Primary School Karatu; Gilbert Sarungi; Institute of Accountancy Arusha; Karatu School Association; Lurelle Vocational Handcraft Training Centre; M & M Kiwera Dispensary; Okutu Primary School Simanjiro; Renea Secondary School; Samaritan Village Tanzania; Toto Aid (NGO); Faraja Young Women; Maroroni Secondary School; Dolly Primary School; Arusha RC's Office; Shuku Foundation; Arusha Mosque; Support + Empowering Women and Sidai Design; na Chalao Secondary School Kilimanjaro.
baadhi ya vifaa hivyo vilivyokabidhiwa.