Mzee                              Shauri Timoth Nathan                               (18/08/1925-18/09/2007)
                Sekunde, Dakika, Saa,                            Siku, Wiki, Mwezi, Mwaka na hatimaye mika saba                            sasa imetimia tangu Mzee Shauri Timoth Nathan                             (18/08/1925-18/09/2007) ututangulie Mbele za                            haki kama ulivyotutangulia kuja duniani Tarehe                            18/08/2025.  
                Nimajonzi                          sana kwetu hasa ukizingatia kuwa uliondoka                          katika tarehe ambayo kitinda mimba wako Mroki                          Mroki alizaliwa na ni siku kumi tu baada ya                          kufunga ndoa Mroki "Father Kidevu".
                Unakumbukwa                          na wengi sana maana ulikuwa ni mhimili mkuu                          katika familia, kipekee ni Mke wako Mary O                          Nathan na watoto wako James Nathan, Mrs Stella                          Kaluse, Lloyd Atenaka, Dossa Mroki,Freddrick                          (Kajiru) Mroki, Onesmo Nathan, Thomas Nathan,                          Daniel Nathan, Kyaze Nathan, Namche Mroki, Kille                          Nathan na Mroki Mroki na Wakwe zako wote.
                Pia                          unakumbukwa sana na Wajukuu zako Kidai Kaluse,                          Shauri Kaluse, Mfaume Kilangi, Shauri James,                          Mwanaamani James, Hellena James, Nuru James,                          Maria Kaluse, Ludao Kaluse, Kilave Atenaka,                          Maria Atenaka, Victoria Dossa, Doureen Atenaka,                          Erick Mushi, Beatrice Mroki, Timothy Tomas,                          Timothy Kajiru, Imanuel Kajiru, Elizabeth                          Kajiru, Timothy Kille, Maria Thomas, Irine                          Atenaka, Anjela Chistian, Glory Mroki, Nathan                          Kyaze, Nathan Dossa, Dinner Onesmo,Digna Onesmo,                          Debora Daniel na  Leonard Kyase pamoja na                          Vitukuu wako pia kutoka kwa Mwanaamani, Kidai na                          Shauri.
                Wananchi                          na majirani zako wa pale Kijiji cha Kipera ,                          Kitongoji cha Kinyenze,Kata na Tarafa ya Mlali ,                          Wilayani Mvomero mkoani Morogoro pia                          wanakukumbuka sana pamoja na wote wa Ugweno,                          Kilimanjaro.
                Tunakumbuka                          maneno yako ya Mwisho uliotuachia watoto wako                          kuwa "TUPENDANE, TUSAIDIANE na TUSHIRIKIANE,"                          baba hakika hili linatendeka na tupo na umoja                          uliotujengea na tunajivunia hilo. 
                Tunazidi                          kukuombea Baraka na pumziko jema maana sote                          uliotuacha tutakufata kama tulivyo kufuata hapa                          duniani.
                Jina la Bwana Lihimidiwe                          Amina.
              
 
