Thursday, July 24, 2014

NDEGE YA ALGERIA IMEANGUKA NCHINI MALI

 
 
 
 
Ndege ya shirika la ndege la Air Algerie ikiwa na watu 116 imeanguka kaskazini mwa Mali. Ilikuwa ikisafiri kutoka Burkina Faso kwenda mji mkuu wa Algeria, Algiers. Kulikuwa na hali mbaya ya hewa katika eneo hilo wakati ilipopoteza mawasiliano na waongoza ndege. Abiria 51 kati ya waliokuwemo ni raia wa Ufaransa. Ndege mbili za kijeshi za Ufaransa zimepelekwa katika eneo hilo kufanya uchuguzi zaidi