Sunday, July 13, 2014

LOUIS VAN GAAL AIAGA VIZURI HOLLAND, YATWAA NAFASI YA TATU …wachezaji wampa zawadi yake, Brazil yalala 3-0



LOUIS VAN GAAL AIAGA VIZURI HOLLAND, YATWAA NAFASI YA TATU …wachezaji wampa zawadi yake, Brazil yalala 3-0
LOUIS VAN GAAL AIAGA VIZURI HOLLAND, YATWAA NAFASI YA            TATU …wachezaji wampa zawadi yake, Brazil yalala 3-0

HOLLAND imefanikiwa kunyakua kitita cha dola milioni 22 baada ya kuinyuka Brazil na kuibuka mshindi wa tatu wa Kombe la dunia 2014.

Brazil iliyoshika nafasi ya nne nayo haitatoka mikono mitupu, inaambulia dola milioni 20.

Celebration: Holland players show off their medals                after beating Brazil in third place play-off

Kikosi cha Holland baada ya kuwa mshindi wa tatu

Holland walifanikiwa kuwabana wenyeji na kupata ushindi wa mabao 3-0 mawili yakitinga katika kipindi cha kwanza na moja kipindi cha pili.

Hii inakuwa zawadi nzuri kwa kocha Loius van Gaal ambaye ameagana rasmi na kikosi hicho akielekea kwenye kibarua chake kipya cha kuikochi Manchester United.

Katika kuelekea mechi hii, Van Gaal aliwaomba wachezaji wake wampe zawadi nzuri ya kumaliza michuano hii bila kufungwa hata mchezo mmoja katika muda wa kawaida (ukiondoa hatua ya bahati nasibu ya mikwaju ya penalti).

Bao la kwanza la Holland lilifungwa na Robin van Persie kwa njia ya penalti kunako dakika ya tatu baada ya Thiago Silva kumwangusha Robben kwenye kisanduku cha hatari.

Dream start: Holland's Robin van Persie scores from                the spot against Brazilian goalkeeper Julio Cesar

 Van Persie akifungua kitabu cha magoli

Cracker: Brazil goalkeeper Julio Cesar fails to save                penalty from Robin van Persie in third minute

 Kipa Julio Cesar anaruka bila mafanikio kuzuia penalti

Joy: Robin van Persie celebrates with team-mate Dirk                Kuyt (up) after scoring the opening goal

Van Persie akishangilia Dirk Kuyt

Beki wa kati wa Holland Daley Blind aliifungia timu yake bao la pili katika dakika ya 17 kufuatia makosa ya David Luiz.

Clinical: Holland defender Daley Blind lashes the                ball into the net for second goal against Brazil

Daley Blind anapachika wavuni bao la pili

Wakati mpira ukionekana utamalizika kwa bao 2-0, Georginio Wijnaldum akaifungia Holland bao la tatu.

Clincher: Holland midfielder Georginio Wijnaldum                seals victory with injury-time strike

 Georginio Wijnaldum akifunga bao la tatu

All together now: Daley Blind (second left)                celebrates scoring Holland's second goal against Brazil

 Holland wanashangilia bao la tatu

Clincher: Holland midfielder Georginio Wijnaldum seals              victory with injury-time strike

 Julio Cesar baada ya bao la tatu

Nightmare: Injured Neymar couldn't bear to watch as              Brazil went down to Holland

Benchi la akiba la Brazil ...huzuni tupu

Brazil: Cesar, Maicon, Silva, Luiz, Maxwell, Gustavo (Fernandinho 46), Paulinho (Hernanes 56), Ramires (Hulk 72), Oscar, Willian, Jo.

Holland: Cillessen (Vorm 90+3), Kuyt, De Vrij, Vlaar, Martins Indi, Blind (Janmaat 70), Clasie (Veltman 89), Wijnaldum, de Guzman , Robben, Van Persie