Wednesday, July 09, 2014

DIWANI WA KATA YA LUPEMBE AFARIKI DUNIA



BREAKING NEWS: DIWANI WA KATA YA LUPEMBE AFARIKI DUNIA


Diwani aliyesimama Bi. Twilumba Wapalila  enzi za uhai wake akiendelea na majukumu yake kama mwakilishi wa wananchi.
 
 Diwani wa kata ya Lupembe wilayani Njombe Bi Twilumba Wapalila, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam alikokuwa akipata matibabu katika hospitali ya Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika zilizopatikana  kutoka kwa viongozi kabla ya kuanza kwa kikao cha baraza la madiwani  la Halmashauri ya Wilaya ya  Njombe wamesema kuwa hii leo watalazimika kufupisha kikao kutokana na msiba huo.





Aidha Baadhi ya wajumbe hao licha ya kuonekana kuwa na simanzi lakini pia wamebainisha kuwa  marehemu alikuwa akisumbuliwa na vidonda vya tumbo.



Msiba huu ni wa pili kwa tarafa ya Lupembe na wa tatu kwa Chama cha mapinduzi Mkoa wa  Njombe  kufuatia siku chache zilizopita aliyekuwa diwani wa kata ya mfiliga kufariki  ikiwa ni siku kadhaa baada ya kutokea kwa msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa chama Hicho Marehemu Adam Msigwa.