Mkuu wa Kitengo cha Risks na Compliance              wa Benki ya Exim, David Lusala (wapili kushoto) akikabidhi              hundi ya shilingi milioni 10 kwa Mweka Hazina wa Tushikamane              Pamoja Foundation (TPF), Ana Rupia (wapili kulia), ikiwa ni              sehemu ya msaada wa benki hiyo kupiga jeki miradi ya TPF ya              kuwasaidia wazee wasiojiweza. Wakishuhudia ni Meneja wa              Fedha Mwandamizi wa Benki ya Exim, Issa Hamisi (katikati) na              Meneja Masoko Msaidizi wa Benki hiyo Anita Goshashy
                Mkuu                wa Kitengo cha Risks na Compliance wa Benki ya Exim, David                Lusala (wapili kushoto) akionyesha hundi ya shilingi                milioni 10  baada ya kukabidhi hundi hiyo kwa Mweka Hazina                wa Tushikamane Pamoja Foundation (TPF), Ana Rupia (wapili                kulia), ikiwa ni sehemu ya msaada wa benki hiyo kupiga                jeki miradi ya TPF ya kuwasaidia wazee wasiojiweza.                Wakishuhudia ni Meneja wa Fedha Mwandamizi wa Benki ya                Exim, Issa Hamisi (kulia) na Meneja Masoko Msaidizi wa                Benki hiyo Anita Goshashy (kushoto).
        BENKI ya Exim Tanzania imekabidhi hundi              ya shilingi milioni kumi kwa taasisi ya Tushikamane Pamoja              Foundation (TPF) ikiwa na lengo la kusaidia wazee              wasiojiweza wanaoishi katika kaya zaidi ya 40 jijini Dar es              Salaam.
        Taasisi hiyo ambayo kwa sasa inasambaza              chakula na vitu binafsi kwa kaya 40 jijini Dar es Salaam              kila mwezi pia utekeleza miradi mbali mbali ambayo ni pamoja              na matibabu kwa kundi hilo maalum.
        Akizungumza wakati wa hafla fupi ya              makabidhiano iliyofanyika katika makao makuu ya benki hiyo              jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Risks na              Compliance wa Benki ya Exim, David Lusala alisema kuwa benki              inajua umuhimu wa kuchangia sehemu ya pato lake kwa jamii,              kwa njia ya miradi ambayo inabadilisha au kuboresha viwango              vya kijamii na kiuchumi kwa jamii.
        "Benki ya Exim imekuwa makini sana katika              kusaidia jamii ianyoizunguka. Kama sehemu ya shughuli zetu              za kijamii, leo tunakabidhi shilingi milioni 10 kwa taasisi              ya TPF ili kupiga jeki miradi yao iliyoanzishwa ili kusaidia              wazee wasiojiweza na jamii kwa ujumla.
        "Nauasa uongozi wa TPF  kuhakikisha kuwa              fedha hizi tulizochangia zinaelekezwa kwenye matumizi              yaliyokusudiwa ili kuwawezesha watu wasiojiweza kufaidika na              shughuli zenu zenye malengo mazuri ya kuboresha maisha yao,"              alisema Bw Lusala.
        Alibainisha kuwa benki ya Exim itaendelea              kuelekeza fedha zake katika kusaidia miradi ambayo ni chachu              ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini ili kusaidia              kuboresha hali ya maisha ya jamii.
        Kwa upande wake, Mweka Hazina wa              Tushikamane Pamoja Foundation, Bi. Ana Rupia ameipongeza              Benki ya Exim kwa msaada wake na kusema kuwa fedha hizo              zilizopokelewa na TPF zitaelekezwa katika miradi ambayo              tayari iliyoundwa kwa lengo la kuwasaidia wazee wasiojiweza.
        "Tuna mpango wa kujenga nyumba kwa ajili              ya wazee katika kata ya Kwembe, Wilayani Kinondoni ambayo              itakuwa kama makazi ya wazee wasiojiweza. Nyumba hiyo itatoa              urahisi wa wazee hao kupata huduma za matibabu, usimamizi wa              karibu na huduma nyingine za kiubinadamu kwa walengwa.
        "Sasa tunasubiri kibali cha ujenzi kabla              ya kuanza kazi ya ujenzi rasmi. Tunaishukuru Benki ya Exim              kwa msaada wao na nazisihi taasisi nyingine kuiga mfano huu              mzuri wa kuigwa," Bi Rupia alisema.
        

 
