Wednesday, September 26, 2012

NAIBU KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE AKUTANA NA WANAJESHI WA AFRIKA KUSINI



 Balozi Rajab Gamaha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akizungumza na Wanajeshi kutoka Chuo cha Taifa cha Kivita cha Afrika Kusini waliofika kutembelea Wizara jana. Mwingine katika picha ni Kanali Shawn Stratsord, Kiongozi wa Wanajeshi hao.
 Baadhi ya Wanajeshi kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza kwa makini Naibu Katibu Mkuu alipozungumza nao.
  Luteni Kanali Sryer, kutoka Chuo cha Taifa cha Kivita cha Afrika Kusini akimkabidhi Balozi Gamaha Tuzo Maalum kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka Chuo hicho.
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Gamaha (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wanajeshi kutoka Afrika Kusini na wenyeji wao wa Tanzania baada ya kuzungumza nao.
Picha na Rosemary Malale wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa