TAMKO LA WAFANYAKAZI
WA MTANDAO WA VIKUNDI VYA WAKULIMA TANZANIA (MVIWATA) KUHUSU MABADILIKO YA
SHERIA YA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII
27 Julai 2012
Sisi
wafanyakazi wa MVIWATA tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya mabadiliko
ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii
yaliyofanywa na bunge mwezi Aprili mwaka 2012 na kusainiwa na Mheshimiwa
Rais Jakaya Kikwete yanayomtaka
mfanyakazi kulipwa mafao yake baada ya kufikisha umri wa miaka 55 hadi 60.
Kwanza,
tunashangazwa iwapo kweli dhamira ya mabadiliko hayo ni kuboresha maslahi ya
mfanyakazi na tunatilia shaka hoja hiyo. Mchakato uliotumika kuibua sheria hiyo
ambao ulikosa uwazi, taarifa zilizopo juu ya hali ya kifedha ya mifuko yenyewe
pamoja na uendeshaji wa mifuko hata kabla ya mabadiliko hayo yanadhihirisha
kwamba dhamira ya marekebisho ya hayo si kwa maslahi ya mfanyakazi.
Kwa
hiyo, tukiwa wafanyakazi wa sekta binafsi, tunaungana na wafanyakazi wenzetu
katika sekta hii wanaopinga kwa nguvu zote sheria hii ambayo utekelezaji wake hautakuwa na
manufaa kwetu wafanyakazi, kwa sababu zifuatazo;
1.
Ajira zetu ni za mikataba ya
muda mfupi na zisizo na uhakika, hivyo mafao ya kujitoa yanamsaidia mfanyakazi
kama mtaji (kianzio cha maisha) mara baada ya kumaliza mkataba wake au kuacha
kazi.
2.
Tukiwa wafanyakazi wa ajira za
mikataba ya muda mfupi mfupi hatuna uhakika wa kupata kazi nyingine mara baada
ya kumaliza mikataba yetu na hivyo kutulazimisha kusubiri hadi kufikia miaka 55
ni kutunyima haki zetu za msingi za kuishi maisha bora. Haki iliyocheleweshwa ni haki
iliyonyang’anywa!!
3.
Mchakato mzima wa kupitisha
mswada mpaka kusainiwa kwa sheria hii haukutushirikisha wamiliki wa mifuko hiyo
ambao ndiyo wachangiaji.
4.
Kwa sababu ya urefu wa muda hadi
kufikisha miaka 55-60 na kwamba mifuko hii ya jamii haina riba, fedha
atakayopatiwa mchangiaji atakapostaafu haiwezi kuwa na thamani iliyonayo wakati
anachangia. Katika hali hiyo malipo ya uzeeni hayamsaidii mchangiaji kupunguza
ugumu wa maisha kama ilivyoelezwa katika ufafanuzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii - Social Security Regulatory Authority (SSRA).
5.
Uzoefu wa wastaafu
waliokuwa wafanyakazi wa Jumuia ya
Afrika Mashariki ambao wamepoteza haki zao mpaka leo unatufanya tusiiamini
mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kwa
hiyo, sisi wafanyakazi wa MVIWATA tunatamka kwa kauli moja kwamba;
1.
Hatukubaliani na mabadiliko hayo
ya sheria na tunapinga vikali utekelezwaji wa sheria ya fao la kujitoa kwani ni
kandamizi.
2.
Tunaitaka serikali ifute mara
moja sheria hii kandamizi yenye lengo la kutunyima wafanyakazi haki zetu na
kutupora maisha yetu.
3.
Tunaunga mkono wabunge wanaotaka
sheria hii ijadiliwe na kurekebishwa ili kulinda maslahi ya wafanyakazi.
4.
Tunakusudia kusitisha michango
yetu katika mifuko ya hifadhi ya jamii iwapo sheria hii haitaondolewa.
Susuma Susuma,
Communication Officer
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA)
E-MAIL: susuma9@yahoo.com, susuma9@hotmail.com, www.mviwata.org
Mobile +255 754 652 773
Tel. +255 23 2614184
Fax. +255 23 2614184
Morogoro
Communication Officer
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA)
E-MAIL: susuma9@yahoo.com, susuma9@hotmail.com, www.mviwata.org
Mobile +255 754 652 773
Tel. +255 23 2614184
Fax. +255 23 2614184
Morogoro