Friday, June 15, 2012

AFARIKI BAADA YA KUGONGWA NA GARI

Trafiki akiwa na wananchi mbele ya mwili wa mtu aliyegongwa na gari na kufa (aliyefunikwa khanga).
Trafiki akiandika maelezo.
Trafiki akishirikiana na wananchi kuubeba mwili na kuupakia kwenye gari.
Wafanyakazi wa Global wakijadiliana jambo mara baada ya ajali hiyo.
Shuhuda wa ajali hiyo akihojiwa na wana habari mara baada ya ajali.
Majira ya saa moja kamili asubuhi ya leo mitaa ya Bamaga jirani na ofisi za gazeti hili mtu mmoja alipoteza maisha papo hapo baada ya kugongwa na gari wakati akiwa anavuka barabara.
Mtu huyo ambaye hakufahamika jina mara moja aligongwa na gari aina ya Toyota Coaster lifanyalo safari zake Mwenge –Posta, kwa mujibu wa shahidi mmoja ambaye hata hivyo alisema hakumbuki namba.

(PICHA HABARI NA HARUNI SANCHAWA/GPL)