Mama mzazi wa marehemu Steven Charles
 Kanumba, Bi. Flora Mtegoa (katikati) akisaidiwa na waombolezaji kuingia
 ndani alipowasili nyumbani kwa mwanae Vatican, Sinza jijini Dar 
akitokea Bukoba mkoani Kagera.
Mama mzazi wa msanii mahiri wa filamu 
nchini, marehemu Steven Kanumba aliyefariki usiku wa kuamkia Jumamosi 
nyumbani kwake Vatican, Sinza jijini Dar es Salaam, Bi Flora Mtegoa, 
jana mchana aliwasili jijini Dar akitokea Bukoba alipokwenda kumjulia 
hali mama yake mzazi anayeishi Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera.
PICHA NA SHAKOOR JONGO/GPL
Kwa Hisani ya GPL. 
 
