Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (katikati) akimpima uzito mtoto Shafii Haji (mwaka mmoja na nusu) mkazi wa Kibugumo Darajani, kama ishara ya kuzindua kambi ya huduma za upimaji afya kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa na Umoja wa Watu kutoka Bengali, India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho) katika shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mratibu wa kambi hiyo kutoka Kliniki ya Al Hilal, Dk. Ali Mzige, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile (wa kwanza kulia) pamoja na Muuguzi wa Zahanati ya Kibugumo, Agnes Mokiwa (wa pili kulia) wakishuhudia tukio hilo.
Meza kuu kwenye uzinduzi wa kambi ya upimaji afya kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa na Umoja wa Watu kutoka Bengali, India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho) katika shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mratibu wa kambi hiyo ya upimaji kutoka Kliniki ya Al Hilal, Dk.Ali Mzige, Mwenyekiti wa Umoja wa Jamii ya watu kutoka India, Bengali waliopo Tanzania (Bango Sangho), Kunal Banerjee, Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Kibugumo, Mzamilo Ally, Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile.(Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile akisisitiza jambo kwenye uzinduzi huo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema kutoa nasaha katika ufunguzi wa kambi hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akitoa neno la ufunguzi wa kambi ya upimaji afya kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa na Umoja wa Watu kutoka Bengali, India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho) katika shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es Salaam.