Tuesday, March 15, 2016

BALOZI WA KUWAIT HAPA NCHINI AMTEMBELEA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI



BALOZI WA KUWAIT HAPA NCHINI AMTEMBELEA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga akimsikiliza Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jassem Alnajem wakati alipomtembelea ofisini kwake Machi 14, 2016. ambapo aliahidi nchi yake kuimarisha zaidi uhusiano na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga akimuelezea Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jassem Alnajem kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara hiyo wakati balozi huyo alipomtembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Machi 14, 2016..
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe. Jassem Alnajem akimkabidhi zawadi ya kumbukumbu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga wakati balozi huyo alipomtembelea Waziri Kitwanga ofisini kwake Machi 14, 2016.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jassem Alnajem wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri Kitwanga ofisini kwake leo. Kulia ni Mwambata wa Ubalozi huo hapa nchini Bw. Mishal Achamidi.