Sunday, April 19, 2015

Wafanyabiashara Songea wasaidia waliokumbwa na maafa.


Wafanyabiashara Songea wasaidia waliokumbwa na maafa.
Wafanyabiashara wa manispaa ya Songea mkoani Ruvuma   kwa kushirikiana na serikali  wamezisaidia  chakula, vifaa  vya ujenzi pamoja na fedha    kaya  kumi na sita zilizokuwa zikilala nje  baada ya nyumba zao kuezuliwa na upepo   katika  kata ya matarawe    mkoani humo.
Mwenyekiti wa jumiya ya wafanyabiashara mkoa wa Ruvuma Bw. Tito Mbilinyi amemkabidhi  katibu  tawala wa wilaya ya songea Bw.Ally Juma vifaa hivyo vikiwa na thamani ya   shilingi  1992,000 ikiwa  pamoja na pesa huku serikali ikiwa imechangia s hilingi  885,000 na kufanya jumla ya pesa zote kuwa milioni mbili elfu themanini na sabini na tano ili awakabidhi wahanga wa  maafa yaliyotokea aprili tano na kuziacha  kaya kumi na sita zikilala  nje.
 
Katibu tawala huyo ameshukuru kwa mchango huo wa wafanyabiashara.
 
Nao wananchi waliokumbwa na maafa hayo matarawe songea  aprili tano siku  ya pasaka wameshukuru kwa msada huo kwa kuwa walikuwa wanalalaa nje.