Tuesday, November 25, 2014

Taarifa ya msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi mstaafu Leonard Mashaka


Taarifa ya msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi mstaafu Leonard Mashaka
Kamishna Msaidizi wa Polisi mstaafu,Marehemu Leonard Mashaka enzi za uhai wake. 

Mheshimiwa Jaji Lillian Mashaka anasikitika kutangaza kifo cha Mume wake Kamishna Msaidizi wa Polisi mstaafu Leonard Mashaka kilichotokea siku ya Jumapili tarehe 23/11/2014. 
Msiba upo nyumbani kwake Mikocheni Dar es Salaam(nyumba za serikali).

Mazishi yatafanyika Jumatano tarehe 26/11/2014.
Ratiba itaanzia nyumbani saa 4 asubuhi na hatimaye misa takatifu katika kanisa la Mt. Martha Mikocheni, Saa 7 mchana.

Mazishi yatafanyika katika makaburi ya Kinondoni (yazamani)kuanzia saa 9 mchana.
Taarifa ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki popote walipo.

Raha ya milele umpe e Bwana na mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani.