Monday, November 10, 2014

BALOZI WA CHINA NCHINI APONGEZA MSIMAMO WA TANZANIA DHIDI YA BIASHARA HARAMU YA PEMBE ZA NDOVU


BALOZI WA CHINA NCHINI APONGEZA MSIMAMO WA TANZANIA DHIDI YA BIASHARA HARAMU YA PEMBE ZA NDOVU
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki akizungumza na Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Lu Youqing alipofika Wizarani tarehe 10 Novemba, 2014 kwa mazungumzo. Katika mazungumzo yao Mhe. Lu aliishukuru na kuipongeza Serikali ya Tanzania kwa msimamo wake kuhusu tuhuma dhidi yake na China kuhusu biashara haramu ya pembe za ndovu na pia alisifu   jitihada za Serikali ya Tanzania katika kupambana na biashara hiyo na kusema China inaunga mkono jitihada hizo na ipo bega kwa bega kuhakikisha inatokomezwa kabisa.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Simba Yahya (wa kwanza kushoto) akiwa na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mbelwa na Balozi Lu (hawapo pichani)
Badhi ya Maafisa kutoka Ubalozi wa China waliofutana na  Balozi Lu wakifuatilia mazungumzo. Picha na Rewben Mchome