![](http://3.bp.blogspot.com/-IZkbRmnyG8w/VFDHFl-58AI/AAAAAAAAt3s/n09cWEqAyNM/s640/Annan-Better.jpg)
Aidha, Annan ameonekana kuvunjwa moyo na jitihada zinazofanywa na mataifa makubwa ikiwemo Marekani kutangaza utaratibu mwisho wa wiki iliyopita wa kuwaweka karantini wauguzi na madaktari waliotoka Afrika Magharibi kwa siku 21, kitu ambacho kinarudisha nyuma ari ya wahudumu hao kujitolea kusaidia wagonjwa kwenye nchi zilizoathirika na Ebola.
Amesema njia pekee ya kuimaliza Ebola ni kufanya jitihada na mapambano ya pamoja katika kuzisaidia nchi za Afrika Magharibi na sio kwingineko, na kuongeza kuwa Afrika inachohitaji ni msaada wa vifaa, madawa na wauguzi ili kupambana na Ebola.
Mpaka sasa Liberia, Guinea na Sierra Leone zimetajwa kuathiriwa zaidi na Ebola,huku takwimu zikionesha zaidi ya watu 4,900 wamefariki na wngine zaidi ya 10,000 kupatwa na maambukizi ya ugonjwa huo.