MASHIRIKISHO YA SANAA NCHINI YATUA BUNGE LA KATIBA KUFUKUZIA HOJA ZAO
MASHIRIKISHO YA SANAA NCHINI YATUA BUNGE LA KATIBA KUFUKUZIA HOJA ZAO
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mh. Samuel Sitta (kulia), akisisitiza jambo kwa wawakilishi wa mashirikisho ya sanaa mjini Dodoma hivi karibuni. Mashirikisho hayo yamekuwa yakipambana kufa na kupona kuhakikisha katiba mpya inatambue wasanii kama kundi maalum na pia ilinde mali zisizoshikika yaani miliki bunifu (intellectual property). Maoni ya mashirikisho hayo yalishatolewa katika hatua za awali za utoaji maoni na pia kupitia mabaraza lakini kwa bahati mbaya, hayakujumuishwa katika rasimu. Waliokaa kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania, Bw. John Kitime, Rais wa Shirikisho la Filamu, Bw. Simon Mwakifwamba na Makamu mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Bi. Samia Suluhu Hassan. (Picha zote kwa hisani ya ofisi ya Bunge la Katiba).