Tuesday, May 13, 2014

VAN GAAL: WAULIZENI MANCHESTER UNITED KUHUSU MIMI

 
 
 
 

Job at hand: Louis van Gaal has deflected questions about his taking over as Manchester United manager

KOCHA wa Holland, Louis van Gaal amekataa kujibu maswali yaliyomuhisha na kibarua cha ukocha wa Manchester United.

Mdachi huyo anajiandaa kurithi nafasi ya David Moyes Old Trafford lakini bado klabu haijatoa taarifa rasmi.

Van Gaal ambaye pia alihusishwa na Tottenham, kwa sasa yuko na kikosi chake cha timu ya taifa ya Holland akikiandaa kwa michuano ya Kombe la Dunia ambapo katika mkutano wake na waandishi wa habari kuelekea kutajwa kwa wachezaji watakaokwenda Brazil, hakuwa katika hali ya kuzungumzia hatma yake.

Focussed: The Holland manager spoke at a pre-World Cup press conference in Hoenderloo on Tuesday

"Hapana, sitasema chochote kuhusu hilo. Niko hapa na kikosi cha Holland. Sio kama kocha wa Manchester United," alisema pale alipoulizwa kuhusu safari ya Old Trafford.

"Mnapaswa kusubiri hadi kila kitu kitakapokamilika au pelekeni maswali hayo kwa Manchester United au pengine klabu nyingi yoyote ile.

"Sitaongea neno lolote kuhusu hilo."