Saturday, October 06, 2012

MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI UVCCM MKOA WA IRINGA KAMANDA UVCCM ASAS ATOA SOMO KWA VIJANA-LIVE



Kamanda  wa UVCCM mkoa  wa Iringa na  Salim Abri Asas akifungua mkutano  huo leo katika ukumbi wa jumba la maendeleo Kitanzini mjini Iringa

wajumbe  wa mkutano mkuu  wa UVCCM mkoa  wa Iringa

Picha ya chini ni .Wagombea  wa nafasi ya uenyekiti UVCCM mkoa  wa Iringa kutoka  kushoto mwanahabari wa Nuru FM Abba Ngilangwa , Mwalimu wa sekondari ya Mwembetogwa Ramadhani Baraza na Mwanahabari wa gazeti la Mwananchi Tumaini Msowoya wakiwa ukumbini leo

Mwanahabari  Tumaini Msowoya anayegombea kiti mkoa  wa Iringa


Kamanda  wa umoja  wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa  wa Iringa Salim Abri Asas ambaye  pia ni mjumbe wa mkutano mkuu  wa CCM mkoa  wa Iringa amewataka  vijana wa CCM mkoa  wa Iringa  kujiajiri wenyewe katika  sekta zisizo rasimi kama njia ya kujikwamua katika maisha.

Amsema hayo  leo wakati  akitoa  salam  zake kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa UVCCM mkoa  wa Iringa  uliofanyika katika ukumbi wa Orofea mjini Iringa .

Asas amesema kuwa  moja kati shughuli ambazo zinaweza kuwakwamua  vijana hao katika dimbwi la umasikini ni pamoja na   kufanya kazi kwa juhudi  zaidi na kuwa na shughuli zao wenyewe za uzalishaji mali.

Hivyo amesema kuwa ili  chama cha mapinduzi CCM kiweze  kuendelea  kuwa mfano kwa vyama vingine vya siasa ni lazima  vijana   wa CCM kuwa mafano kwa vijana wa vyama vingine ikiwa ni pamoja na  kufanya kazi kwa  juhudi  zaidi badala ya  kushinda vijiweni katika makundi ambayo hayana faida katika Taifa.