Saturday, October 11, 2014

MH. MAHENGE AFANYA ZIARA KATIKA MGODI WA NORTH MARA




MH. MAHENGE AFANYA ZIARA KATIKA MGODI WA NORTH MARA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mhe. Dkt. Binillith S.Mahenge akipewa maelezo na Mkuu wa Wilaya ya Tarime alipowasili ofisini kwake kabla ya kuanza ziara ya kikazi katika Mgodi wa North Mara ulioko Wilaya ya Tarime.
Meneja wa Mazingira Mgodi wa North Mara Bwana Thomas Morris akitoa Maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mhe. Dkt. Binillith S.Mahenge (hayupo pichani) alipotembelea Mgodi wa North Mara kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira katika maeneo ya migodi nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mhe. Dkt. Binillith S.Mahenge (wa tatu kutoka kushoto) akipewa maelezo na Meneja Mazingira Bwana Thomas Morris kuhusu mitambo ya kuteketeza taka zenye sumu zinazozalishwa katika mgodi wa North Mara. Wa pili kushoto ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Bwana Gary Chapman.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mhe. Dkt. Binillith S.Mahenge akipewa maelezo ni jinsi gani wanavyoweza kusafisha Maji kwa Mitambo ya kisasa katika Mgodi wa North Mara.