Friday, October 10, 2014

Rais Kikwete aweka jiwe la Msingi Barabara Usagara -Kisesa,pia afunngua Daraja la Mabatini


Rais Kikwete aweka jiwe la Msingi Barabara Usagara -Kisesa,pia afunngua Daraja la Mabatini
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya kilometa 16 kutoka Usagara hadi Kisesa mkoani Mwanza leo.Rais Kikwete yupo mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua daraja la Nyashishi lenye urefu wa mita 67 lililopo katika barabara ya Usagara Kisesa wakati alipokwenda kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara kilometa 16 ya Kisesa hadi Usagara inayojengwa kwa kiwango cha lami leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzibdua rasmi daraja la waenda kwa miguu Mabatini Mkoani Mwanza leo.Wapili kushoto ni Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli.
Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli akimuongoza Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kukagua daraja la waenda kwa miguu huko Mabatini Mkoani Mwanza leo muda mfupi baada ya kulifungua leo.
Muonekano wa Daraja la waenda kwa miguu liliojengwa Mabatini huko Mwanza lililozinduliwa na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo. (picha na Freddy Maro)