Naibu Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Bw. Andy Mwandembwa amepokea msaada wa vifaa mbali mbali kwa ajili ya watanzania wenye ulemavu wa ngozi wanaofanya shughuli za ujasiriamali kutoka kwa Mwanadiaspora mkereketwa anayeishi Sweden, Bw. Mbarouk Rashidi. Msaada huo unajumisha vifaa vya ufundi wa karakana, nguo, vitabu na vitendea kazi vingine.