Leo ni miaka miwili sasa tokea Mpendwa wetu VICTORIA,uliposikia sauti ya Mungu wetu ikikuita nawe ukaitika. Bado tunakukumbuka kwa namna ya pekee kwa Ucheshi, Upendo na Upole.Kwetu kumbukumbu hizi ni hazina zetu.
Victoria unakumbukwa sana na mimi mama yako LYDIA,Baba yako mlezi mpendwa Japheth Mbwana,Mumeo mpenzi Emmanuel Kilato, Ndugu zako Godfrey, Mercy, Viollah, na wengine wengi sana kama Mama mkubwa, Wajomba zako, Wakwe zako, wanaukoo wote,Majirani wa Lumala,- Mwanza,Geita,Dodoma, Walimu wako wa Shule, na Chuo UDOM, wafanyakazi wa Benki kuu Mwanza,wanaparokia ya Pasiansi Mwanza,Wanaparokia wa Pasiansi – Mwanza,Wanajumuiya wa Mt.Fidel – Lumala Mwanza,Ndugu jamaa na marafiki hasa Masista wa Poor Clares wa Nyanguingi Mwanza.
MWENYEZI MUNGU AKUANGAZIE MWANGA WA MILELE UPUMZIKE KWA AMANI.AMINA.