Wednesday, June 11, 2014

MHE. MEMBE ASHIRIKI KATIKA SHEREHE ZA KUMUAPISHA RAIS WA MISRI



MHE. MEMBE ASHIRIKI KATIKA SHEREHE ZA KUMUAPISHA RAIS WA MISRI
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) (kulia) akiwa katiika Kiwanja cha Ndege cha Addis Ababa  akiwa njiani kuelekea Cairo, Misri katika sherehe za kumuapisha Rais Mteule, Mhe. Abdel Fattah al Sisi. Mwingine katika picha ni Bw, Shelukindo, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Waziri Membe (kushoto)  akiongea na Msaidizi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ambaye ana ngazi ya Ukurugenzi kwenye chumba cha Wageni Maalum katika Uwanja wa Ndege wa Cairo alipowasili kwa ajili ya kushiriki sherehe za kumuapisha Rais wa nchi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje (kulia) akipokea taarifa fupi kutoka kwa Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Misri, Bw. Jestas Nyamanga katika Hoteli aliyofikia Mhe. Waziri ya Fairmont.
Mhe. Waziri Membe mwenye miwani akiwa amesimama mbele ya Hoteli ili kuingia katika gari maalum kwa ajili ya kumpeleka eneo lililofanyika sherehe za uapisho. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Vincent Kibwana.