Tuesday, May 24, 2016

WALIOGHUSHI NYARAKA ZA NHIF WATUPWA JELA MIAKA 27


WALIOGHUSHI NYARAKA ZA NHIF WATUPWA JELA MIAKA 27
Mkaguzi wa NHIF, Charles Mjema akizunguza na waandishi wetu  juu ya hukumu ya iliyotolewa leo katika mahakama ya Ilala kwa watu wawili waliohukumiwa kwenda jela miaka 27 kwa makosa ya kugushi nyaraka za NHIF za kujipatia dawa katika madauka ya dawa yaliyosajiliwa na NHIF leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
WATU wawili wamehukumiwa kwenda jela kwa makosa ya kugushi nyaraka za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)  za kuweza kujipatia dawa katika maduka ya dawa yaliyosajiliwa na mfuko huo.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Ilala, Mhe. Juma Hassan ambaye alidai mahakamani hapo kuwa washitakiwa wote  wawili watatumikia jela kutokana na makosa yao tisa ambapo mtuhuhumiwa wa kwanza Bakari Ramadhan amehukumiwa miaka 27 jela kwa makosa yote tisa na Ahmed Mohamed amehukumiwa miaka 12 kwenda jela kwa makosa manne.
Washitakiwa hao walikamatwa Desemba 14 , 2014 katika Duka JD Pharmance lilopo Posta wakiwa wanataka kuchukua dawa na kabla ya kukamatwa.
Akizungumzia hukumu hiyo Mkaguzi wa NHIF, Charles Mjema amesema kuwa wananchi watumie mfumo uliowekwa na NHIF na sio kughushi kutokana na mifumo iliyopo inabaini watu walio halali wa kuchukua dawa.
Amesema kuwa NHIF imeweka utaratibu wa mtu kuweza kupata matibabu na kupata dawa katika mfumo ulio bora kughushi hakuwezi kuwasaidia na akifanikiwa kufanya hivyo jela ina mwita.