Monday, April 25, 2016

TAHMEF YATOA HUDUMA YA UPIMAJI WA AFYA BURE KUELEKEA SIKU YA MALARIA DUNIANI



TAHMEF YATOA HUDUMA YA UPIMAJI WA AFYA BURE KUELEKEA SIKU YA MALARIA DUNIANI
Kuelekea siku ya Malaria Duniani ambayo kitaifa huadhimshwa tarehe 25 Aprili, Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF) limetoa huduma ya upimaji wa Afya tarehe 23 Aprili katika msikiti wa Masjid Al Ghadir, uliopo Kigogo, Jijini Dar es salaam.

Huduma hiyo ilihusisha upimaji wa Malaria, kisukari, shinikizo la damu na upungufu wa damu, ambapo Matibabu ya Dawa na ushauri ulitolewa kwa wananchi waliobainika kuwa maradhi hayo, chini ya uangalizi wa madaktari wazoefu.

Jumla ya wananchi 352 walipata huduma hii, wanawake wakiwa 150 na wanaume 202 kati ya idadi hiyo.
Mkazi wa kigogo akipata Huduma ya upimaji Wa Afya katika zoezi lililoendeshwa na TAHMEF.
Muanzilishi wa TAHMEF, Bi. Juliana Busasi (aliembeba mtoto) akisaidia katika kufanikisha upimaji wa malaria kwa mtoto ambaye ni mkazi Wa kigogo.