Monday, June 30, 2014

Super Eagles wayaaga mashindano kwa kutandikwa 2-0 na Ufaransa



...and Nigeria did not advance to the quarter-final stage
France just beat Nigeria 2-0 to advance to the quarter-final stage of the 2014 World Cup! France played well, and many feel they deserved the win...but our Super Eagles did well too! Especially, goal keeper Vincent Enyeama. He's been our saviour in this tournament. Thank you!

What did you think of the match? And the own goal by Nigerian captain, Joseph Yobo? I think he played well. I also think Enyeama deserves African Footballer of the Year 2014. What do you think?


Global value chains amplify requirements for structural transformation in Africa



Global value chains amplify requirements for structural transformation in Africa



Mtangazaji Regina Mwalekwa Aikimbia Clouds FM, Apata Deal la Nguvu Redio Kubwa




Mtangazaji Regina Mwalekwa Aikimbia Clouds FM, Apata Deal la Nguvu Redio Kubwa
Leo Asubuhi Mtangazaji wa Clouds FM Mwanadada Regina Mwalekwa Ametangaza wazi kwenye kipindi cha Power Breakfast cha Clouds FM kuwa anaacha kazi rasmi katika kituo hicho alichofanya kwa muda mrefu, Regina Mwalekwa aliwashukuru Watangazaji na Mabosi wa Kituo cha Clouds kwa Kumlea Vizuri katika kipindi chote alichokuwa hapo.
Regina Mwalekwa hakusita kusema sababu ya Kuacha kazi kituo hicho ambapo alisema amepata kazi katika Shirika la Utangazaji la BBC.


Raisa ndie Redds Miss Kanda ya Kaskazini




raisa ndie redds miss kanda ya kaskazini
 hawa ndio washindi wa redd's miss kanda ya kaskazini kwa mwaka 2014


 hawa ni wadhimini wa shindano hilo kutoka minjingu

Lemutuzz nae alikuwemo ndani ya Redd's miss kanda ya kaskazini  bila kumsahau mwenyekiti wa Taswa Juma pinto


 mkuu wa mkoa wa Arusha pamoja na mkuu wa mkoa wa Manyara waliuthuria katika usiku huo wa kumsaka mrembo wa kanda ya kaskazini ambapo katika shindano hilo warembo wanne wamwanzo watakingia katika kambi ya Redd's miss Tanzania
 mh hashimu Lundenga akiwa anatangaza washindi wa tatu bora
 watembo wakiwa wameingia ukumbini wakicheza wimbo wa ufunguzi





 papa mwandago akimwaga maneno akiwa kama muandaaji mkuu wa shindano hili

 hawa ndio warembo walioingia tano bora

 waandaji wa shindano hilo wakiwa wamekaa kwa mapozi wakifuatilia shindano. PICHA zote na libeneke la kaskazini blog



NHIF YATETA NA WADAU WAKE WA MKOA WA DAR ES SALAAM




NHIF YATETA NA WADAU WAKE WA MKOA WA DAR ES SALAAM
1Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Mkuu wa Waya ya Ilala Mh. Raymond Mushi akifungua mkutano wa Wadau wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya NHIF uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Malimu Nyerere Conference Centre jijini Dar es salaam kuzingumzia mambo mbalimbali kuhusu huduma hiyo ya bima ya afya, wadau waliohudhuria katika mkutano huo n kutoka wilaya ya Temeke, Ilala na Kinondoni mkoani Dar es salaam, Lengo kuu likiwa kuhamasisha na wananchi kujiunga na mfuko huo na kufikia asilimia 30% ifikapo mwaka 2015, Pia kuangalia changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa malengo hayo na kuzitatua.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM) 2Kamimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya Bw. Khamis Mdee akizungumza na kuelezea mikakati ya mfuko huo kwa wadau waliohudhuria katika mkutano huo leo. 3Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Bima ya Taifa Afya ya Jamii NHIF Balozi Ally Mchumo akimkaribisha mgeni rasmi ili kuzungumza na wadau wa mfuko huo. 4Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Mkuu wa Waya ya Ilala Mh. Raymond Mushi kushoto akiwa katika meza kuu wakati wa mkutano huo kulia ni Jason Blasius Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Katikati ni Teresia Mbando Katibu Tawala mkoa wa Dar es salaam. 5Mkurugenzi wa Idara ya Masoko na Utafiti kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Raphael Mwamoto akiteta jambo na mmoja wa wadau wa mfuko huo. 6Baahi ya wadau waliohudhuria katika mkutano huo 7 8 9Mbunge wa jimbo la Kigamboni Dr. Faustine Ndungulile akiwa katika mkutano huo. 10Anjela Mziray (kushoto) Meneja masoko kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya akisoma taarifa za mkutano huo ulipokuwa ukiendelea. 11Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Mkuu wa Waya ya Ilala Mh. Raymond Mushi na viongozi wa mfuko huo wakipig picha na wadau mbalimbali walioshiriki katika mkutano huo. 12 13 14 15Kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na Mkuu wa Waya ya Ilala Mh. Raymond Mushi akihijiwa na vyombo mbalimbali vya habari mara baada ya kufungua mkutano huo


KAGASHEKI CUP 2014: TIMU YA KAGONDO YAITUNGUA BUHEMBE FC BAO 1-0



KAGASHEKI CUP 2014: TIMU YA KAGONDO YAITUNGUA BUHEMBE FC BAO 1-0
Na Faustine Ruta, Bukoba.
Timu ya Kagondo FC imejipatia Alama tatu muhimu kwenye Mtanange wao dhidi ya timu ya Buhembe FC leo kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba Mjini kwenye Michuano ya Kombe la Kagasheki. Bao hilo la pekee lilifungwa na Mchezaji namba tisa Mgongoni Abduratif Khamis katika kipindi cha kwanza dakika 37. Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa bao hilo 1-0 na kipindi cha pili timu zote mbili hakuna iliyoziona nyavu za mwezake timu licha ya kushambuliana mara kwa mara. Mwamuzi alipuliza kipenga dakika 90 kumaliza mtanange huo na Timu ya Kagondo FC wakiibuka na ushindi huo wa bao 1-0. Mapema leo Mchana Timu ya Nshambya na Kibeta ziliumana na timu zote mbili zilimaliza mtanange kwa sare ya bila kufungana kwa kutoka 0-0. Kesho Ligi hii inaendelea tena kwa siku ya nne na kutakuwepo na michezo miwili, Mapema ni Nyanga vs Kitendaguro na Jioni saa 10:00 ni Wagonga Nyundo "Ijuganyondo Vs Kahororo".
Kikosi cha Timu ya Kagondo Fc
Kikosi cha Timu ya Buhembe FC
Timu Kapteni na waamuzi wakiteta kabla ya Mpambano hii leo kwenye uwanja wa Kaitaba,Bukoba Mjini
Kipute kilianza kwa Timu ya Buhembe kwa kasi sana
Kila Mtu na wake!
Patashika katikati ya uwanja
Wachezaji wa Timu ya Kagondo Fc wakishangilia bao lao lililofungwa na Abduratif Khamis katika dakika ya 37 kipindi cha kwanza. kulia ni kipa wao nae alikuja kuwapongeza!!!
Mtanange ulikiendelea kipindi cha pili...
Frii kiki kuelekea kwenye lango la Kagondo FC
Mchezaji wa Kagondo aliumia, Watoa huduma ya kwanza wakimpa msaada wa kumtoa nje ya uwanja kwa matibabu
Lakini aliumia na kadi yake ya Njano ilimfata huko huko nje!
Kipa wa Kagodo chupuchupu afungwe bao hapa katika kipindi cha pili. Kipindi cha pili hakuna aliyeziona nyavu za mwenzake bao hilo lilidumu mpaka dakika za mwisho
Hatari: Kipa wa Kagondo Fc akidaka mpira wa Kona
Kipindi cha Pili dakika za mwishoni Timu ya Buhembe FC ilipata kona mbili lakini haikuweza kusawazisha bao, licha ya kuliandama lango la wenzao Kagondo Fc.
Kipa akipangua mpira uliopigwa kwa kona..dakika za mwishoni.


AJTC BINGWA WA BONANZA LA TISA LA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA KASKAZINI



AJTC BINGWA WA BONANZA LA TISA LA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA KASKAZINI

mwenyekiti wa Taswa Taifa Juma  Pinto akiwa akiwa anakagua timu ya mpira wa pete kutoka AJTC kabla ya mechi ya fainaili kuchezwa

washabiki wa timu ya AJTC wakiwa wanashangilia mara baada yakukabidhiwa kombe katika bonanza la Taswa


Meneja masoko wa Mega trade, Godluck Kway akitoa  neno ndani ya bonanza hilo


Mkuu wa matukio ya kanda ya kaskazini Bw. Christ Sarakana kutoka TBL akiongozana na meneja masoko na mauzo wa kampuni ya Mega Trade Investment Godluck Kway kukagua timu ya netball ya chuo cha uandishi wa habari AJTC



 

IMG-20140629-WA0000kikosi cha timu ya mpira wa miguu kutoka cho cha AJTC



IMG-20140629-WA0002


IMG-20140629-WA0003Nahodha wa timu ya mpira wa miguu wa AJTC Bw. Alli Ahmedi akikabidhiwa kombe la ubingwa na Mkuu wa matukio ya kanda ya kaskazini Bw. Christ Sarakana kutoka TBL

IMG-20140629-WA0004

Timu za Chuo Cha Uandishi wa Habari Arusha (AJTC) juzi zilitwaa ubingwa katika bonanza la tisa la waandishi wa habari Kanda ya Kaskazini, lililofanyika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Katika bonanza hilo, ambalo mgeni rasmi alikuwa, Mwenyekiti wa Taswa Taifa, Juma Pinto  jumla ya timu  10 zilishiriki na  liliandaliwa na Taswa Arusha kwa ushirikiano na kampuni ya Ms Unique.

Timu ya soka ya AJTC ilitwaa ubingwa baada ya kuifunga kwa mikwaju ya penati 5-4 timu ya Radio Sunrise, wakati wasichana wa timu hiyo, waliwashinda timu ya chuo cha  uandishi wa habari na maendeleo ya jamii (IMS), magoli 18-5.

Mgeni rasmi Pinto ambaye pia ni Mjumbe wa bodi vya Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro alikabidhi vikombe na fedha taslimu, ambapo bingwa wa  soka alipewa kikombe, pamoja na fedha taslimu 200,000 na seti ya jezi.

Mshindi wa pili wa soka akipata 100, 000 wakati bingwa wa mpira wa pete alizawadiwa kikombe na fedha taslimu 100, 000 huku mshindi wa pili akikabidhiwa tsh 50, 000.

Katika bonanza hilo, ambalo lilidhaminiwa na kampuni ya bia nchini, (TBL), kampuni ya Megatrade Investment, Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro, Cocacola, SBC (T) ltd, AICC, Tanzanite Forever, TANAPA na Alphatel,

Timu zilizoshiriki ni Radio 5, timu ya Arusha One, ORS kutoka mkoa wa Manyara, Salam Club, IMS na  Taswa Arusha  ambayo iliibuka na ushindi katika kukamata kuku.

Akizungumza katika bonanza hilo, Pinto alipongeza washindi na viongozi wa Taswa Arusha kwa kazi  nzuri waliofanya.

"Nachukuwa fursa hii kuwapongeza sana Taswa Arusha kwa kuandaa bonanza hili kwani halifanyiki sehemu nyingine nchini"alisema

Awali Meneja matukio wa TBl, Chris Sarakana aliahidi TBL kuendelea kudhamini bonanza hilo kutokana na kuvutia wanahabari na wakazi wengi wa Arusha.

Meneja masoko wa Mega trade, Godluck Kway aliwapongeza wanahabari kwa kushiriki kwa wingi katika bonanza hilo na kuahidi kuendelea kulidhamini.