Wednesday, November 19, 2014

BENKI YA NMB MBEYA YATEMBELEA KITUO CHA YATIMA CHA MALEZI YA HURUMA NA KUTOA MISAADA MBALI MBALI.


BENKI YA NMB MBEYA YATEMBELEA KITUO CHA YATIMA CHA MALEZI YA HURUMA NA KUTOA MISAADA MBALI MBALI.
Maafisa wa Benki ya NMB Mbeya wakishusha vitu kutoka kwenye gari kwa ajili ya kukabidhi msaada katika kituo cha watoto yatima Malezi ya Huruma Simike.

Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Mbalizi Road, Mzee Mwakibete, akikabidhi msaada kwa wanafunzi wa kituo cha watoto yatima cha Malezi ya Huruma Simike Mbeya.


Afisa biashara wa NMB Tawi la Mbalizi Road, Alex Massawe, akikabidhi msaada kwa wanafunzi wa kituo cha watoto yatima cha Malezi ya Huruma Simike Mbeya.

Mmoja kati ya Watumishi wa NMB tawi la Mbalizi Road akikabidhi msaada kwa wanafunzi wa kituo cha watoto yatima cha Malezi ya Huruma Simike Mbeya.


 Watumishi wa Benki ya NMB wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhi msaada.


Mmiliki wa kituo cha Malezi ya Huruma, Anah Kasire akitoa shukrani kwa niaba ya watoto.

WAFANYAKAZI wa Benki  ya Nmb tawi la Mbalizi road Mbeya wametembelea kituo cha watoto  yatima cha Malezi ya Huruma kilichopo Simike jijini Mbeya na kutoa misaada mbali mbali yenye thamani ya shilingi Milioni 1.1.

Afisa biashara wa NMB Tawi la Mbalizi Road, Alex Masawe alisema msaada waliotuo ni kutokana na wafanyakazi wa Benki hiyo kuguswa na maombi ya mmiliki wa Kituo hicho akiomba msaada wa vifaa vya shule kwa watoto wawili wanaoenda vyuo vya ualimu.

Alivitaja vitu vilivyopelekwa kuwa ni pamoja na Matranka mawili, makufuri mawili, Mchele debe tatu, mashuka 4, sabuni katoni 4, mafuta ya kula lita 20,sabuni ya unga kilo 20,nguo za ndani dazani 2, free style moja, mafuta ya kupaka dazani 2,miswaki dazani 5 na dawa za mswaki dazani 4.

Vingine ni vitambaa kwa ajili ya sare za chuo vya rangi nyeusi mita 6, mashati mawili, sabuni za kuogea dazani mbili, makaratasi aina ya manira 10, blanketi 4,unga wa sembe kilo 20, mahindi debe tatu, nyanya sado moja na vitunguu sado moja.

Masawe alisema hivyo vitu baadhi yake vitasaidia kituo na vingine ni kwa ajili ya wanafunzi waokwenda kusoma ambao sambamba na vitu hivyo pia walikabidhiwa fedha taslimu shilingi Laki moja na kufanya jumla ya vitu vilivyotolewa kuwa na thamani ya shilingi milioni 1.1.

bidii
Kwa upande wake Mmiliki wa Kituo hicho, Annah 
Kasire mbali na kuipongeza benki ya NMB kwa msaada huo alisema vitu hivyo vitaleta chachu kwa wanafunzi kuongeza katika masomo yao.

Aliwataja wanafunzi wanoenda kusoma kuwa ni Magreth Mwasile na Tumain Mwampamba ambao wote kwa pamoja wanatarajia kwenda kusoma Chuo cha Ualimu kilichopo Nyororo mkoani Iringa na kuongeza kuwa hadi sasa kituo kinalea watoto 120.

Mwisho.
Na Mbeya yetu