Tuesday, December 06, 2011

Kumbukumbu ya Brigedia Gen. Moses Nnauye leo!

Ni miaka kumi sasa tangu ututoke mzee nnauye. Mapenzi yako yaliyotukuka kwa nchi yako yataendelea kukumbukwa milele. Ulikuwa amana ya Mungu kwa familia yako na taifa zima kiujumla, leo Mungu ameichukua amana hiyo toka kwetu, hatuna cha kulaumu bali kushukuru kwani kazi ya mungu haina makosa na kila nafsi itayaonja mauti, tulikupenda sana comrade lakini mapenzi yetu kwako hayakufua dafu mbele ya mapenzi ya mungu kwako.

Mke wako Mwanaisha, watoto wako Nape, Mariam, Joseph, Winnie, Mwate, Samora, Mussa na Bimdo wanakukumbuka na kukuombea sana kwa mungu. Wakwe zako January, Peter,Paul na Grace wanakukumbuka pia. Wajukuu zako Selemani, Adam, Otilia, Sanya, Kareen, Frank Jr wanakukumbuka pia.

Marafiki zako na watanzania kwa ujumla pia wanakukumbuka sana mzee Nnauye.

INNALILAAAHI WA INNAILAIHI RAAJIUUM!
Source: www.jamiiforums.com