Friday, January 30, 2009

Bodi ya Mikopo hiyooooooooooo

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imefanya mabadiliko ya utaratibu wa utoaji mikopo kwamba, sasa watatoa asilimia 100 kwa wanafunzi wa vitivo mbalimbali kulingana na vipaumbele vya serikali.


Makamu Mwenyekiti wa bodi hiyo, Nicolaus Mbwanji, alisema jana kuwa utaratibu huo utaanza kutumika katika mwaka mpya wa fedha wa 2009/2010 kwa kuanzia na wanafunzi wa fani za sayansi.


Katika marekebisho hayo bodi hiyo imeongeza makundi yatakayopata mikopo kutoka sita hadi 11, pamoja na kutoa mikopo ya kujiendeleza kwa wahadhiri wa vyuo binafsi sawa na wale wa serikali.


Akizungumza jana jijini Mwanza alisema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kutembelea vyuo 17 na kuzungumza na wanafunzi, viongozi wa serikali zao na wakuu wa vyuo hivyo.

Alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu, bodi hiyo ilikuwa ikitoa mikopo kwa makundi na asilimia zake katika mabano A(100), B(80), C(60), D(40), E(20) na F(0), lakini sasa imeongeza idadi ya makundi hayo hadi kufikia 11, ambayo ni na viwango vyake vya asilimia za mkopo katika mabano A(100), B(90), C(80), D(70), E(60), F(50), G(40), H(30), I(20), J(10) na K(0).


Alisema lengo la mabadiliko hayo ni kuondoa pengo kutoka kundi moja hadi lingine na kuleta uwiano mzuri katika makundi ya uchangiaji na kuwa sasa mikopo haitatolewa kwa kufuata madaraja ya viwango vya kufaulu vinavyotumika sasa (daraja la kwanza na la pili).


"Kwa sasa utoaji mikopo hautafuata 'division' (daraja), bali utakuwa ukizingatia udahili wa wanafunzi katika vyuo na kwa utaratibu huu, chuo kitapewa idadi ya wanafunzi watakaokopeshwa kulingana na programu zake na idadi itapangwa kulingana na vipaumbele vya taifa, kama itakavyoelekezwa na serikali, ikiwemo elimu na sayansi," alieleza.


Mbwanji alifahamisha kuwa katika mwaka wa fedha wa 2009/2010, bodi yake itatoa kipaumbele kwa wadahili wote wa sayansi ambapo watapewa mkopo kwa asilimia 100, hii ni kutokana na wanafunzi wa sayansi ambao wamekuwa wakinufaika na mkopo kuwa pungufu ya asilimi 35.


Marekebisho mengine ambayo bodi imefanya ni kuongeza kiwango cha mikopo kwa vitabu na viandikwa (stationary) kutoka sh. 120,000 ya sasa hadi kufikia 200,000 kwa mwaka kwa wanafunzi wote.


"Eneo lingine ni ulipaji wa ada kwa maombi ya mikopo, katika mabadiliko haya itatozwa sh. 30,000 mara moja kwa mwaka wa kwanza, badala ya utaratibu wa nyuma wa kutoza kwa kila mwaka.


Mabadiliko mengine ni utoaji mikopo kwa wahadhiri wa vyuo vya elimu ya juu binafsi, kwa ajili ya kusoma shahada za uzamili na uzamivu. Hawa pia watapewa badala ya wale wa serikali pekee.” alisema.


Akielezea mabadiliko hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, George Nyatega alisema wanafunzi watakaopata mikopo watapaswa kupitishwa na bodi za elimu za kijiji, kata, tarafa na wakuu wa wilaya, ili kuwatambua zaidi na kuepuka udanganyifu kwa waombaji.


Hata hivyo alisema kuwa, utaratibu huo mpya umepelekwa serikalini kwa ajili ya kuthibitishwa na kwamba, utaanza kutumika mwaka huu kwa wadahiliwa wapya na kwamba, waliopo vyuoni sasa wataendelea na utaratibu wa zamani mpaka watakapohitimu masomo yao.


Alisema katika kufanikisha mpango huo mpya, bodi yake inatarajiwa kudahili wanafunzi 60,000 watakaokopeshwa ikiwa ni zaidi ya mwaka jana walipodahili 55,685 na kwamba, mwaka huu wanatarajia kutumia kiasi cha Sh175 bilioni.


Hadi kufikia mwaka jana bodi ilikuwa imekopesha jumla ya sh 62.2 bilioni kwa wanafunzi 56,07. Wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaosoma nchini ni 23,061, wanoendelea na masomo 32,012 na wanaosoma nje ya nchi ni wanafunzi 998.


Jijini Dar es Salaam, Benjamain Sawe na Zawadi Msalla wanaripoti kuwa, Mkurugenzi wa Usambazaji wa Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu, Lubambula Machunda amewashauri wanafunzi kufuata utaratibu uliowekwa na bodi ya mikopo nchini, ikiwa ni pamoja na kufuta vigezo sahihi vilivyopangwa katika kufuatilia madai na matatizo mbalimbali yanayoshughulikiwa na bodi hiyo.


Alisema bodi imejiandaa kufungua ofisi zake katika kila kanda na kwamba, wataanzia Dodoma na Zanzibar, lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na vyuo.


Alivishukuru vyuo mbalimbali nchini kwa kutoa maofisa wake katika kukusanya matatizo ya wanafunzi, kuhusiana na mikopo na kuyashughulikia kwa utaratibu uliopangwa na bodi hiyo.


Sera mpya ya uchangiaji elimu ya juu, ambayo iliweka mfumo wa kutoa mikopo kufuatana na makundi, imesababisha wanafunzi kugoma kwa madai kuwa unalenga kuwanyima haki watoto wa masikini kupata elimu ya juu na hatimaye vyuo kufungwa.


Wanafunzi hao pia waliitaka serikali itoe mikopo kwa asilimia 100 kwa wanafunzi wote na vitivo vyote, badala ya kutenga makundi ambayo hata hivyo, hayazingatiwi kutokana na baadhi ya watoto wa wenye uwezo kulipiwa zote na wale wa masikini wakiwekwa kwenye makundi ya kuchangia.


Hata hivyo hivi sasa vyuo vikuu vya umma vilivyokuwa vimefungwa, vinaendelea kudahili upya, ingawa hatua hiyo imekuwa ikipingwa na wanafunzi.

Jamani eeeeeeeee PM atokwa na chozi Bugeni.


Machozi ya Pinda yalowesha wabunge
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifuta machozi wakati akielezea mauaji ya Albino alipokuwa akijibu swali Bungeni kuhusiana na kauli yake aliyoitoa hivi karibuni katika mikoa ya kanda ya ziwa.Hoja ya wapinzani kumtaka ajiuzulu yayeyuka
Leon Bahati
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alio nao dhidi ya vitendo vya mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), hivyo kuyeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji ambayo ni kinyume na katiba ya nchi.
Hali hiyo ilitokea jana bungeni, wakati Pinda akielezea yaliyomfanya atoe kauli hiyo tata kikatiba na misingi ya haki za binadamu.
Pinda alisema alipokuwa katika ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alipata taarifa za kusikitisha kuhusu mauji ya albino na mara kesho yake habari zikatoka kwenye vyombo vya habari kwamba, albino mwinge kauawa.
"Jamani jamani taarifa za matukio hayo kibinadamu zinatia uchungu sana na kumfanya mtu ashindwe kujizuia….," mara akaanza kutokwa machozi na kukatisha maelezo yake akatoa miwani na kujifuta huku wabunge wakiwa kimya.
Waziri Mkuu alisema hayo baada ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed, kumtaka atoe ufafanuzi kuhusu kauli aliyoitoa hivi karibuni akiwa katika ziara Kanda ya Ziwa, kuwaruhusu wananchi kuwaua watu watakaokutwa wakimchinja albino.
Hamadi alisema katiba ya nchi inamlinda mtu kupewa nafasi ya kujitetea, hivyo akamtaka waziri afafanue maana ya kauli yake, kwa kuwa ni kinyume na taratibu ambazo nchi imejiwekea katika kuhakikisha haki inapatikana.
Pinda alisema mtu anaposikia au kusoma taarifa za mauaji ya albino, hawezi kupata hisia juu ya mateso wanayoyapata, sawa na anayewasikiliza watu walionusurika kufa au walioshuhudia vitendo hivyo vikitendeka.
“Mimi walinihadithia, aah! Samahani," alisema kwa masikitiko Pinda huku akiwataka radhi wabunge kwa kushindwa kuendelea kueleza kwa jinsi alivyoguswa na matukio hayo. Mara akaanza kububujikwa na machozi na baada ya sekunde kama 15, alichukua kitambaa chake akajifuta.
Aliendelea kuelezea jinsi maalbino wanavyouawa kikatili, akisema wengi walikufa kwa kushindwa kupata huduma mapema ya kuzuia damu baada ya ama kukatwa mikono ama miguu na majitu hayo katili yenye imani potofu kwamba, viungo hivyo vinaweza kumpatia mtu utajiri.
Alisema alielezwa kuwa, wauaji wanachokifanya ni kumshambulia albino na kumkata kiungo wanachokitaka kwa kutojali hali wanayomuacha nayo kama ni mateso, kufa au kupona hivyo alipatwa na uchungu kiasi cha kujikuta anatamka kuwa, watu wanaokutwa wakitenda hayo nao wanapaswa kuadhibiwa papo hapo.
Alifafanua kuwa wakati akiwa kwenye ziara hiyo iliyokuwa maalumu kwa ajili ya kukemea na kupanga mikakati ya kukabaliana na vitendo hivyo, idadi ya maalbino waliouawa walikuwa 30 na baada ya kukemea vitendo hivyo, ghafla akapewa ripoti ya kuuawa wengine wawili, jambo ambalo lilizidi kumuudhi na kumchanganya.
Waziri Pinda aliwaomba radhi watu walioudhika kutokana na matamshi na pia akimuomba Mungu amsamehe iwapo amewakosea.
"Kama mnaona kile nilichofanya ni makosa naomba mnivumilie. Naomba Mungu anisamehe kama nimewakosea," aliomba Waziri Mkuu na kuongeza kuwa serikali imechukizwa sana na mauaji hayo ya kikatili.
Alisema Tanzania imekuwa ikiheshimika sana katika jumuiya ya kimataifa, lakini mauaji ya albino na ya vikongwe katika eneo hilo yameitia doa.
Alielezea pia kuhuzunishwa zaidi na tamko la Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) la kulaani mauaji hayo, kana kwamba wao wanaguswa sana na suala hilo kuliko Serikali ya Tanzania.
Hata hivyo, alisema kuwa katika ziara hiyo, ambayo iliwahusisha pia baadhi ya mawaziri, wabunge, viongozi wa polisi, viongozi wa dini na kisiasa, waliahidi kushirikiana kuhakikisha kuwa wanakabiliana na kulimaliza tatizo.
Isitoshe alisema aliwataka viongozi wa vijiji kurejesha ulinzi wa jadi, maarufu kama sungusungu ili kukabiliana na wauaji.
Pinda alisema kuwa serikali ipo tayari kupokea maoni kutoka kwa watu mbalimbali, yanayoweza kusaidia kupata mbinu ya kukomesha kabisa mauaji hayo, ili kuiokoa jamii hiyo ya albino.
Alisema katika kumbukumbu za serikali, hadi mwishoni mwa mwaka jana vikongwe 2,866 walikuwa wameuawa kwa imani potofu kuwa ni wachawi.
Alisema serikali imeliagiza jeshi la polisi kutumia maarifa yake, hata kama itabidi kutumia gharama kubwa, ili kuwatia mbaroni watu wote wanaojihusisha na mauaji hayo.
Wapinzani pia walimtaka Pinda atoe maelezo yanayodaiwa kuwa yalitolewa na Rais Jakaya Kikwete kisiwani Pemba kwamba, aliwashangaa wakazi wa eneo hilo kuwachagua watu ambao hawawezi kuunda serikali na ambao watachukua muda mrefu kupata nafasi hiyo.
Pinda alisema anapata taabu kujibu swali hilo, kwa sababu hawezi kuyatolea maelezo mambo yaliyozungumzwa na bosi wake na wala hajui kama ni kweli rais alisema kama vyombo vya habari vilivyoripoti.
Mbunge wa Konde, Dk Ali Tarab Ali (CUF) alimtaka Pinda aeleze kama kitendo cha Rais Kikwete kutumia magari ya serikali kisiwani Pemba na kuonekana akifanya shughuli za chama ni matumizi mabaya ya fedha za serikali.
Pinda alimjibu akisema kuwa, ni vigumu rais kutofautisha vyombo vya usafiri anavyovitumia wakati akifanya ziara za kisiasa ama za kiserikali na kutoa mfano kwamba, hata rais wa Marekani hutumia ndege aina ya Air Force one bila kuchagua kuwa ni shughuli ya kisiasa au kiserikali.
Wakati hayo yakitokea bungeni, baadhi ya viongozi wa dini nchini, wamemtaka Waziri Pinda kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi.
Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam, Sheikh Ramadhan Sanze alisema Pinda alifanya kosa la kiufundi kwa kuwa yeye ni mtendaji mkuu wa serikali, hivyo hakupaswa kusema jambo linalopingana na msimamo wa serikali, sheria na katiba ya nchi.
"Kwa vile kauli hiyo haijaleta madhara mpaka sasa Waziri Mkuu ana uchochoro wa kupita ili kujisafisha. Cha msingi ni kukiri kosa, kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa mamlaka za kisheria, Bunge na Wananchi" alishauri Sheikh Sanze.
Alisema, hajafuatilia vizuri kuhusu hoja za kambi ya upinzani bungeni na kwamba, kujiuzulu inaweza isiwe suluhisho la tatizo hilo kwa kuwa, hata kama atajiuzulu kauli haitafutika na tatizo litabaki palepale.
"Nchi hii haina dini na kwa hiyo haingozwi na sheria za dini bali inaongozwa na sheria za nchi, kwa hiyo Pinda alipaswa kuangalia sheria ya nchi kwanza kabla ya kutoa agizo lake," alisema Sheikh Sanze.
Alifafanua kuwa, Waziri Pinda ametengeneza mazingira ya uchafuzi na uchochezi, kutokana na kauli yake hiyo kwani baadhi ya watu wanaweza kuitumia vibaya kwa kumuua mtu kwa sababu ya chuki tu baina yao.
Alisema, athari ya kauli kama hizo zinaweza kusababisha migogoro kati ya dini na dini nyingine, kabila moja na jingine au dhehebu moja na jingine kama wananchi watautumia wito huo.
Alisema vita dhidi ya mauaji ya albino imekuwa ikitumika kisiasa zaidi kuliko kitaalamu na kuongeza kuwa, mamlaka husika ziliangalie tatizo hilo kitaalamu badala ya kuliacha likitumika kisiasa.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Valentino Mokiwa alisema kauli ya Pinda ya kutaka aliyeua albino auawe si sahihi kwa sababu mtu akimuua aliyeua ni muuaji na ana kosa kisheria.
Mauaji ya albino yamekuwa yakitikisa nchi na hasa katika eneo la Kanda ya Ziwa, licha ya juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali kupitia jeshi la polisi, mashirika ya kutetea haki za binadamu, vyama vya walemavu na watu binafsi.

Thursday, January 29, 2009

Majinafasi ya kazi. Sasa ushindwe wewe tu.

Engineering & Technical Services Manager - Asset IntegrityOur client is a major provider of integrity engineering, inspection management, inspection and NDT services to the Petrochemical, Utility, Oil and Gas and Power Generation industries. A vacancy has arisen for a Chartered Engineering & Technical Services Manager to join their Senior Management Team...Salary: c£80k - £100kpa + Benefits (Negotiable) . Location: UK . Job type: Permanent . Company: JAM Recruitment Ltd. . Date posted: 27 Jan 2009 18:05
View full job details and apply

Production Delivery Rail EngineerProduction Delivery Engineer - Location - Slade GreenTo motivate and lead an engineering team, prioritise and manage workloads, liaising with other departments as necessaryYou will need to be able to provide technical expertise for the team and SPM, including, troubleshooting and defect...Location: Slade Green, Erith (DA8) . Job type: Permanent . Company: Joy Recruitment . Date posted: 27 Jan 2009 16:35

Mradi wa magari yaendayo kasi kujenga barabara za zege Dar

Dar sasa ni Tambarare,

Hebu soma kisa hiki....................

Mradi wa Magari yaendayo kasi jijini Dar es Salaam (DART) unatarajia kuanza kujenga barabara kwa kutumia zege badala ya lami, zitakazotumika kupitisha magari hayo ambapo dola za Marekani milioni 122.1, sawa na Sh. bilioni 150 zinatarajia kutumika. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtendaji Mkuu wa DART, Cosmas Takule, alisema kutokana na uimara wa barabara hizo za zege, wana uhakika wa kudumu kati ya miaka 20 hadi 30 bila kufanyiwa matengenezo yoyote. Huduma za magari hayo zitaanza Novemba mwakani. Alisema barabara za lami zinadumu kati ya miaka mitano hadi tisa kama hazikufanyiwa matengenezo. Kadhalika, alisema mradi huo utajumuisha ujenzi wa maeneo ya maegesho ya magari jijini Dar es Salaam. Alisema mradi huo utakapokamilika utasaidia kupunguza msongamano wa magari, tatizo ambalo limekuwa sugu hivi sasa jijini Daer es Salaam. Alisema katika awamu ya kwanza ya mradi, watajenga barabara kuanzia Kimara hadi kivukoni jijini Dar es Salaam na kwamba hakuna gari yoyote itakayoruhusiwa kupita hapo zaidi ya magari yaendayo kasi. Alifafanua kuwa barabara hiyo itakuwa na vituo vitano kutoka mwanzo hadi mwisho. Takule alisema hawatatenga eneo jipya la kujenga barabara hizo bali zitakuwa sambamba na ile ya Morogoro inayotoka Kimara hadi kati kati ya jiji la Dar es Salaam. Aidha, baadhi ya barabara zitaongezwa na kufanywa ziwe za kwenda bila magari kupishana (oneway). Aidha, alisema wataweka barabAra za juu katika makutano ya barabra za Mandela, Sam Nujoma na ile ya Nyerere. Takule aliwataka wananchi kuamimini kwamba mradi huo upo na tayari serikali imetoa Sh. bilioni 10 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi watakaobomolewa nyumba zao zilizopo kando kando mwa zitakapopita barabara hizo. Kwa upande mwingine alisema kutakuwa na magari ya mzunguko kuanzia eneo la Wazo, Kunduchi, Mwenge, Tabata, Uwanja wa Ndege, Mbagala na kuishia Kigamboni jijini Dar es Salaam. Kuhusu mkandarasi alisema, DART ipo katika mchakato wa kumtafuta na kwamba mara baada ya kumpata, ujenzi utaanza muda wowote.
SOURCE: Nipashe

Wednesday, January 28, 2009